Thursday, August 21, 2014

Je, Walimu wetu wameandaliwa kuikomboa jamii?

      Walimu  ni  kundi  muhimu  katika  jamii  ambalo  huchangia  sana  katika  malezi  ya  watoto kimawazo,  kiakili  na  kiuelewa.


Hapa  Tanzania  mwalimu  anatambulika  kama  mtu  aliyefuzu  mafunzo  ya  ualimu  na  kutunukiwa cheti.  lakini  je  cheti  pekee  kinatosha  kuonyesha  mwalimu  bora?.  Mwalimu  ni  muwezeshaji  na muongozaji  wa  mawazo  ya  mwanafunzi,  kuyakuza  na  kuyastawiisha  pamoja  na  kuuboresha ubunifu  wa  mwanafunzi.


Mwalimu  bora  ni  yupi?.  Mwalimu  bora  ni  yule  mwenye  mbinu  mbalimbali  za  kuhakikisha mwanafunzi  anabaki  darasani  kimawazo  na  kiakili  kivitendo  zaidi.  Elimu  si  madarasa,  madawati  na  ufundishaji  tu  bali  ni  uwezo  wa  motto  kuelewa  anachojifunza.


Huyu  ndiye  mwalimu  anatayekomboa  jamii.


"Education is the most powerful weapon which you can use to change the world ." - Nelson Mandela

0 comments:

Post a Comment